0
Kwa muda mrefu Diva wa muziki wa Bongo Flava ambaye anajulikana kwa ufundi wake wa kucheza na sauti, Judith ‘Ladyjaydee’ Wambura, alikuwa kimya kikazi (muziki) mpaka hivi juzi alipoamua kuachia hit inayosumbua vituo kadhaa vya radio nchini ‘Ndi ndi ndi’.
Star huyu naweza sema amerudi kwa mshindo mkuu, na hata style aliyoitumia kurejea nayo mimi kama mdau wa muziki niliielewa sana, nazungumzia ule msemo wa ‘Naamka tena’.
Sasa jana Jaydee akizungumza kupitia kipindi cha Twenzetu cha Times Fm, ameelezea jinsi alivyopata Idea ya kutumia msemo huo na jinsi ulivyobamba kitaani.
Jide amedai yeye na timu yake walikaa kuzungumza ni jinsi gani wanarudi, na katika mawazo yote yaliyowekwa kujadiliwa mezani ndipo wakakubaliana kutumia ‘Naamka tena’.
“Unajua kuamkaa si lazima uwe ulifumba macho, atakama ulikaa unaweza sema naamka tena, nilikaa kimya kwa muda mrefu sasa tukaamua tu hii ije mara moja ‘naamka tena’ nashukuru msemo ulikuwa mkubwa sana huu” Alisema.

Chapisha Maoni

 
Top